GABON NJE AFCON 2017

Tokeo la picha la GABON AFCON 2017 IMAGE

WENYEJI Gabon wametupwa nje ya AFCON 2017, Mashindano ya 31 ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, baada ya kutoka Sare 0-0 na Cameroon huko Libreville katika Mechi yao ya mwisho ya Kundi A.
 
Sasa Cameroon na Burkina Faso, ambao Jana waliifunga Guinea-Bissau 2-0, wamesonga Robo Fainali huku Burkinabe wakiwa Washindi wa Kwanza wa Kundi na Cameroon ni wa Pili.

Nchi nyingine ambazo zimetinga Robo Fainali wakiwa na Mechi 1 mkononi ni Senegal na Ghana.

Leo zipo Mechi za mwisho za Kundi B ambapo Senegal watacheza na Algeria na Zimbabwe kuivaa Tunisia huku Algeria na Tunisia zikisaka kuungana na Senegal Robo Fainali na Zimbabwe ikikamilisha Ratiba tu.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment