JE KLOPP ATAFUFUA MATUMAINI KWA MASHABIKI WA LIVERPOOL LEO?

Tokeo la picha la livepool vs chelsea match preview image

MENEJA wa Liverpool Jürgen Klopp amesisitiza Msimu wao haujapotea na Timu yake inaweza kufufua matumaini ya Ubingwa kwa Leo kuwafunga Chelsea Uwanjani Anfield kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.
 
Liverpool wameporomoka hadi Nafasi ya 4 kwenye EPL wakiwa Pointi 10 nyuma ya Vinara Chelsea walio chini ya Meneja Antonio Conte.
 
Ndani ya Wiki moja iliyopita, Liverpool wametupwa nje ya Makombe Mawili, EFL CUP na FA CUP, wakipokea vipigo vitatu mfululizo Nyumbani kwao Anfield ambako hawajafungwa Mechi 4 mfululizo tangu Mwaka 1923.
 
Kipigo cha 4 hakitaki Klopp na safari hii anacheza na Chelsea ambayo Mwezi Septemba aliichapa huko Stamford Bridge Bao 2-1.
 
Baada ya kurejea kwa Sadio Mane kikosini akitokea huko Gabon kwenye AFCON 2017 alikokuwa akiichezea Nchi yake Senegal, Klopp anaweza kuwachezesha kwa pamoja kwa mara ya kwanza tangu Novemba 6 walipoinyuka Watford 6-1, Mastaa wake kina Sadio Mané, Philippe Coutinho, Roberto Firmino na Adam Lallana ambao ni kombinesheni kali ya Mashambulizi.
 
VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
 
Liverpool: Mignolet, Clyne, Lovren, Klavan, Milner, Henderson, Can, Firmino, Coutinho, Lallana, Mane
 
Chelsea: Courtois, Azpilicueta, Luiz, Cahill, Moses, Matic, Kante, Alonso, Hazard, Pedro, Costa
 Tokeo la picha la Mark Clattenburg IMAGE
                             Mark Clattenburg

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment