MABINGWA wa La Liga huko Spain, FC Barcelona, Jana waliifyeka Las
Palmas 5-0 na kukamata Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 2 tu nyuma ya Vinara
Real Madrid.
Lakini Real wana Mechi 2 mkononi na Leo wana nafasi ya kuliongeza
pengo la Pointi kuwa 5 wakicheza Ugenini na Sevilla ambayo Juzi
ilishindwa kuibwaga Real dhaifu iliyocheza bila Wachezaji kadhaa maarufu
akiwemo Mchezaji Bora Duniani Cristiano Ronaldo walipoumwaga uongozi wa
3-1 na Real kurudisha na kuwa 3-3 katika Mechi ya Pili ya Raundi ya
Mtoano ya Timu 16 ya Copa del Rey.
Real, wakiwa pia na Timu dhaifu, waliinyuka Sevilla 3-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Copa del Rey.
Bao za Barca hiyo Jana zilifungwa na Luis Suarez, Bao 2, Lionel Messi, Arda Turan na Aleix Vidal.
Mapema Jana, Bao la Dakika ya 8 la Nicolas Gaitan liliipa Atletico Madrid ushindi wa 1-0 walipocheza na Real Betis.
0 Maoni:
Post a Comment