ALEXIS SANCHEZ AMEKIRI UDANGANYIFU WA KODI HISPANIA.

Tokeo la picha la ALEXIS SANCHEZ IMAGE
FOWADI wa Arsenal Alexis Sanchez amekiri kwa Mamlaka ya Kodi huko Spain wa kukwepa Kodi ya €983 443 wakati akiichezea Barcelona.
 
Sanchez, Mchezaji wa Kimataifa wa Chile mwenye Miaka 28, sasa anakabiliwa na kupigwa Faini na pengine Kifungo ambacho kinaweza kuwa cha nje.
Akitoa ushahidi wake akiwa Jijini London, England, Sanchez alikubali 'kosa katika stahili ya Malipo ya Kodi yake' ambayo sasa amelipa yote.
Sanchez amekiri kuwa hesabu za Kodi yake za Miaka ya 2012 na 2013 hazikujumuisha Faida iliyotokana na Umiliki wake wa Picha na Matangazo yake ambayo yalilipwa kupitia Kampuni yake iliyokuwa huko Malta.
Tokeo la picha la ALEXIS SANCHEZ IMAGE
Pia Sanchez alikiri kumiliki Kampuni hiyo Numidia Trading Limited ambayo hakuibanisha kwenye Malipo ya Kodi zake huko Spain.
Kesi hii inafanana na ile ya Mchezaji wa Barcelona Javier Mascherano ambae Januari 2016 alipigwa Faini €815 000 na Kifungo cha Mwaka Mmoja alichotumikia nje ya Gereza kwa udanganyifu wa Malipo ya Kodi huko Spain.
Wengine waliokumbwa na kadhia kama hiyo ni Staa wa Barcelona na Argentina Lionel Messi na Baba yake Mzazi kutwangwa Faini ya Euro Milioni 2 hapo Julai 2016 na pia kuhukumiwa kufungwa Jela Miezi 21 Kifungo ambacho kilifanywa kiwe cha nje badala ya Gerezani.
Huko Spain Vifungo vya chini ya Miaka Miwili hutumikiwa nje ya Gereza.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment