POLISI WAMTIA MBARONI GRANIT XHAKA.

Tokeo la picha la XHAKA IMAGE OF RED CARD

KIUNGO wa Arsenal Granit Xhaka amehojiwa na Polisi baada ya kuibuka tuhuma za kumkashifu kibaguzi Mfanyakazi wa Kampuni ya Ndege Uwanjani Heathrow Jijini London.
 
Xhaka, Raia wa Uswisi mwenye Miaka 24, anaaminika kuwa alikuwa akimsindikiza Rafiki yake aliemtembelea London na kukutwa na mkasa huo Jumatatu Usiku.

Sakata hilo linadaiwa kutokea baada ya Mchezaji huyo wa Arsenal na Rafikiye kuchelewa kufika Uwanja wa Ndege na Rafiki huyo kuzuiwa kupanda Ndege kurejea Ujerumani.

Hapo ndipo inadaiwa Xhaka alitoa maneno ya kashfa ya Kibaguzi na Polisi wamethibitisha kutokea tukio hilo na kusema Mtuhumiwa amehojiwa na uchunguzi unaendelea.
Klabu ya Arsenal imekataa kuzungumza lolote.

Tukio hili la Xhaka limetokea takriban Masaa 24 tangu apewe Kadi Nyekundu kwenye Mechi ya Ligi na Burnley ambayo Mswisi huyo alitolewa kwa Kadi Nyekundu wakati Arsenal inashinda 2-1 kwenye Mechi ambayo pia Meneja wa Arsenal Arsene Wenger alitolewa nje ya Uwanja na Refa na Jana kushitakiwa kwa Utovu wa Nidhamu na FA, Chama cha Soka England.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment