IBRAHIMOVIC NA MINGS KUSULUBIWA NA PILATO WA FA, KUFUNGIWA?

 Tokeo la picha la ibrahimovic na mings image

LEO REFA Kevin Friend ataonyesha kama ni rafiki au la wakati akiwasilisha Ripoti yake ya Mechi aliyochezesha Jumamosi kati ya Manchester United na Bournemouth huko Old Trafford na kuishia kwa Sare ya 1-1.
 
Mbali ya Zlatan Ibrahimovic kukosa Penati katika Mechi hiyo iliyojaa matukio mengi ikiwemo la Refa huyo kutoa Kadi ya Njano kwa Mchezaji wa Bournemouth Andrew Surman na ‘kusahau’ kuwa hiyo ni Kadi ya Njano ya Pili na kupita Dakika kadhaa ndipo ‘alipokumbuka’ na hivyo kumuwasha Kadi Nyekundu, tukio kubwa ni ‘vita’ kati ya Sentahafu wa Bournemouth Tyrone Mings na Straika wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic.
  Tokeo la picha la ibrahimovic na mings image

Vita hiyo ilifikia wakati Refa Kevin Friend kuwaonya wote Wawili lakini ikafikia kilele pale Mings alipomtimba Kichwani Ibrahimovic aliekuwa ameanguka katika Dakika ya 44 na Dakika 2 baadae Ibrahimovic alionekana ‘kumpiga kiwiko’ Mings wakati akipiga Kichwa Mpira wa Kona.

Wachezaji wote hao Wawili wamejitetea kuwa matukio hayo si ya kusudi.

Lakini kinachofuatia ni nini kimeandikwa kwenye Ripoti ya Refa Friend ambayo Leo itatua Mezani kwa FA, Chama cha Soka England.

Ikiwa Refa huyo atakiri kuwa aliyaona Matukio hayo Mawili basi stori inakwisha hapohapo kwani FA hawawezi tena kuchukua hatua zaidi.

Lakini ikiwa Refa Friend atakuwa si rafiki tena akidai hakuyaona au kutotaja chochote kwenye Ripoti yake basi FA, kwa mujibu wa Kanuni, wanaweza kuamua kupeleka Matukio hayo Mawili kwa Jopo Huru la Marefa wa Zamani Watatu ambao watayapitia na kuamua kama yalistahili Kadi Nyekundu au la.

Wakiamua ni Kadi Nyekundu basi FA itatoa Kifungo cha Mechi 3 au zaidi ikitegemea uzito wa kila Kosa.
Ikiwa atafungiwa basi Ibrahimovic atazikosa Mechi ya Robo Fainali ya FA CUP dhidi ya Chelsea na Mechi za Ligi dhidi ya Middlesbrough na West Bromwich Albion.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment