ARSENAL YATUPWA NJE YA MASHINDANO YA EFL

efl

Magoli ya Jordy Clasie na Ryan Bertrand yameitupa nje Arsenal kwenye kombe la EFL na kuipeleka Southampton hatua ya nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1987.
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger ambaye hajawahi kutwaa taji hilo katika miaka yake 20 aliyoishi London, alifanya mabadiliko ya wachezaji 10 kwenye kikosi cha Arsenal kilichoshinda 3-1 dhidi ya Bournemouth kwenye mchezo wa Premier League Jumapili iliyopita.
Southampton ambao wameshinda mara moja katika michezo 23 waliyosafiri kuifata Arsena, walistahili ushindi na watacheza dhidi ya Liverpool kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza itakayochezwa kwenye uwanja wa St Mary January 9 mwaka ujao.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment