OLD TRAFFORD KUINGIZA WALEMAVU WENGI UWANJANI BAADA YA MAREKEBISHO.


Tokeo la picha la old trafford image

MANCHESTER UNITED imetangaza kuubadili Uwanja wao wa Old Trafford ili kuruhusu Walemavu wengi kupata nafasi ya kuingia Uwanjani.

Mipango hiyo itafanya uwezo wa Uwanja huo mkubwa kabisa England kupita Klabu yeyote kushuka kutoka Watu zaidi ya 75,000 na kuwa takriban Watu 73,300.

Taarifa hiyo imetamka kuwa ukarabati kamili kuwezesha Walemavu kuingia ndani Uwanjani kirahisi ambao kwa sasa upo Jukwaa la Mashariki tu ukipanuliwa na kuwa hadi Majukwaa ya Sir Alex Ferguson na Sir Bobby Charlton.
 Tokeo la picha la old trafford image

Lakini mipango hiyo itaathiri baadhi ya Washabiki wa Man United wenye Tiketi za Msimu mzima kuingia Old Trafford ambao watalazimika kuhamishiwa maeneo mengine Uwanja hapo huku wakipewa fidia ya kuona Mechi za Makombe bure.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment