UFAHAMU MFUMO WA 3-4-3 UNAVYOFANYA KAZI HADI KUWA GUMZO KWA CHELSEA

3-4-3

KATIKA soka sasa stori kubwa hasa nchini Uingereza ni mfumo wa 3-4-3 unaoonekana kuipa matokeo mazuri klabu ya Chelsea. Basi leo tutauangalia kidogo mfumo huo tupate kuufahamu hapa.

Kwa asili huu ni mfumo ambao waingereza wanasema <very offensive mind> yaani wakushambulia zaidi ambao asili yake ni huko Uholanzi 1970 katika klabu ya Ajax.

Walianzisha mfumo huu kwa lengo la kutoa fursa ya kushambulia katika maumbo tofauti tofauti. Unaweza kuwa Flat 3-4-3 au diamond 3-4-3 au wowote ambao utatokana na kocha mwenyewe.

ULINZI

MFUMO wa 3-4-3 unaifanya safu ya ulinzi kuwa imara sana ikiwa na mabeki wa tatu dhidi ya washambuliaji wa kati lakini unaweza kufanya mpinzani apate nafasi hasa pembeni kama hakuna watu wazuri wakuziba nafasi hizo.
Hivyo mfumo huo unataka kiungo mkabaji mzuri pia awe anaasili ya ku-hold/kutunza mipira isipotee hovyo ili kuwalinda mabeki na kuongeza kuwa mabeki wanne pindi inapohitajika.
Lakini pia inataka washambuliaji wa pembeni wazuri wanaoweza kuziba nafasi za pembeni na kupandisha mashambulizi. 

Diagram A

3-4-3
Kiungo X8 anapaswa kuwa mkabaji sana na mlinzi wakati X4 ni mchukua mipira na kuipeleka mbele/mchezeshaji.
Pembeni viungo X6 na X7 kazi yao ni kutoa msaada mbele kwenye mashambulizi lakini pia kurudi nyuma zaidi kuongeza walinzi na X8 ataziba nafasi ya kati.

Ushambuliaji katika 3-4-3

Mfumo wa 3-4-3unatoa nafasi kwa timu kuwa na washambuliaji watatu.
Hivyo kwa sababu ya kuwa na washambuliaji watatu kunawapa nafasi ya kuwa na wachezaji wengi ambao wengine wanaweza kuwa katika nafasi ya kupokea pasi za kupitishwa nyuma ya mabeki a.k.a through passs.
Wakati X9 anatoa cross basi X10 anakuwa mbele ya goli ili kutia presha na X11 anakuwa mkimbiaji mwenye kutafuta nafasi ya goli mara nyingi anakuwa huru mfano Eden Hazard kwa Chelsea.

Ubora wa mfumo:

  • Washambuliaji mara nyingi wanakuwa mbele kutafuta goli.
  • Viungo anne wanatoa uhai kwa timu katikati na hata mbele na nyuma.
  • Washambuliaji na viungo wanaweza kuchezesha timu kila upande na kuwachanga wapinzani wao hasa mabeki wasijue wakumkaba.
  • Walinzi wanakuwa imara sana dhidi ya washambuliaji wa kati.
Udhaifu wa mfumo:

  • Huu mfumo wa kujipanga kama umbo la almasi maarufu kama The diamond midfield formation unaweza kutoa nafasi kwa timu nyingine kuzitumia kutokana na kuwa gaps nyingi endapo hakuna wachezaji wanaoendana na mfumo huu.
  • Mabeki au walinzi wakiwa watatu wanaweza kuwa rahisi kuchanganywa na wachezaji wenye kasi wanaobadilishana nafasi.
Image result for 3-4-3 formation

Mahitaji ya mfumo

  • Mabeki wenye kasi na wenye uwezo kimwili na kiafya kuziba nafasi ya beki wanne.
  • Viungo wakabaji wazuri wenye kuwa na uwezo wa kuzuia mipira ya mashambulizi ya kushtukiza pia waporaji wazuri wa mipira.
  • Washambuliaji wenye kuweza kuendesha mipira mbele ikiwezekana kasi na uwezo binafsi wakupunguza walinzi pindi inapohitajika.
  • Zaidi ni mawasiliano mazuir kati ya walinzi na viungo ili kuwa na ulinzi mzuri.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment