KOCHA JUVENTUS AKATAA PONGEZI

 

Licha ya ushindi mujarabu wa 2-1 dhidi ya Monaco, kocha wa Juventus Massimilliano Allegri amekataa pongezi za aina yoyote na kusema kufanya vizuri ni wajibu wake .
 
Allegri ambaye ameipa ushindi mnono Juventus kwa jumla ya goli 4-1 kwa michezo yote miwili ya nusu fainali kwenda fainali ya klabu bingwa ulaya, amekwenda mbali zaidi na kusema anapenda kufundisha na anapenda matokeo mazuri lakini hapendi kusifiwa pale anapotimiza wajibu wake.

”Mi kwa imani yangu pongezi zifanyike kwa mtu au jambo ambalo lina asili ya uajabu lakini sio majukumu ya msingi ya mtu” alieleza kocha huyo ambaye anasifika kwa misimamo mikali.

“I try to do my work serenely and with enthusiasm, but I’m not interested in the others saying that I’m the best. I really enjoy coaching, it helps me relax and when it starts to cause me stress, I will stop.”

Wakati anawasili Juventus mwaka 2014 mashabiki wa timu hiyo hawakuwa na mapenzi nae na walimkaribisha kishingo upande akitoka kufungwa na wababe wa Italy AC Milan.

Allegri alikuja Juventus kuchukua nafasi ya Antonie Conte. Msimu wa kwanza na Juventus mashabiki wakiwa hawamtaki aliwashangaza kwa ushindi wa kombe la ligi na kuwapeleka michuano ya klabu bingwa ulaya akifanya hivyo mara mbili jambo lililoanza kumfanya apendwe na mashabiki hao na siku zote yeye akikataa sifa zao na kusema ubora wa timu ni sehemu ya majukumu yake .

”wasifuni wachezaji kuelewa mbinu zangu na kuipa mafanikio timu yenu. Sifa kwangu hazina maana yoyote bali niombeeni tu niendelee kutekeleza majukumu yangu katika ubora wake” alieleza kocha huyo.

Kukataa sifa na kusimamia misimamo yake pia kutojisifu mbele ya vyombo vya habari humfanya Allegri kuwa kocha wa kipekee na kivutio kwa wengi.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment