JE CHELSEA KUTANGAZA UBINGWA LEO??

 Picha inayohusiana

LEO Chelsea wapo The Hawthorns kucheza na West Bromwich Albion wakijua ushindi kwao utawapa Ubingwa wa EPL, LIGI KUU ENGLAND huku wakiwa na Mechi 2 mkononi.
 
Chelsea wanaongoza Ligi hii wakiwa na Pointi 84 kwa Mechi 35 wakibakiza Mechi 3 na Timu pekee inayoweza kuwakamata ni Tottenham Hotspur ambao wana Pointi 77 kwa Mechi 35.

Ikiwa Chelsea watashinda hii Leo watafikisha Pointi 87 ambazo Tottenham hawawezi kuzifikia.

Hii Leo Chelsea wanacheza na WBA ambayo waliifunga katika Mechi ya Kwanza na ambayo ipo Nafasi ya 8 ikiwa salama salimini kwenye vita ya kujinusuru kushuka Daraja.

Kila Timu inatarajiwa kuwa na Kikosi kamili na Kiungo wa Chelsea, N'Golo Kante, anatarajiwa kucheza baada ya Jumatatu iliyopita kuikosa Mechi na Middlesbrough akiwa na maumivu ya Paja.

Kante ndie ambaye ametwaa Tuzo za Mchezaji Bora zilizotolewa na PFA na FWA, Vyama vya Wachezaji wa Kulipwa na kile cha Waandishi wa Soka.

Mechi nyingine ya EPL hii Leo ni huko Goodison Park kati ya Everton na Watford.

EPL, LIGI KUU ENGLAND
Ratiba:

Ijumaa Mei 12
2145 Everton v Watford              
2200 West Bromwich Albion v Chelsea   
          
Jumamosi Mei 13
1430 Manchester City v Leicester City             
1700 Bournemouth v Burnley                
1700 Middlesbrough v Southampton     
1700 Sunderland v Swansea City 
1930 Stoke City v Arsenal  

Jumapili Mei 14
1400 Crystal Palace v Hull City    
1615 West Ham United v Liverpool       
1830 Tottenham Hotspur v Manchester United 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment