WATU 10 WAIADHIRI MOROCCO AFCON 2017.

Tokeo la picha la CONGO DR VS MOROCCO IMAGE
CONGO DR Jana waliifunga Morocco 1-0 katika Mechi ya Kundi C la AFCON 2017, Mashindano ya 31 ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, kwenye Mechi iliyochezwa huko Stade d'Oyem, Assok Ngomo Nchini Gabon.
 
Bao la ushindi la Congo DR, ambao Wiki iliyopita walifanya mgomo kushinikiza kulipwa Fedha zao, lilifungwa na Junior Kabananga katika Dakika ya 55.
Tokeo la picha la CONGO DR VS MOROCCO IMAGE

Congo DR walibaki Mtu 10 kuanzia Dakika ya 81 kufuatia Kadi Nyekundu kwa Lomalisa Mutambala, alieingizwa kutoka Benchi, na ndani ya Dakika 16 kupewa Kadi za Njano 2.

Mapema Jana, kwenye Mechi nyingine ya Kundi C, Mabingwa Watetezi Ivory Coast walitoka 0-0 na Togo. Leo Jumanne zipo Mechi mbili za Kundi D kati ya Ghana na Uganda na kisha ni Mali na Egypt zote zikichezwa Oyem Stadium, Mjini Assok Ngomo huko Gabon.

VIKOSI VILIVYOANZA:

CONGO DR: Matampi, Nsakala, Zakuani, Tisserand, Ssama, Mulumba, Bope Mbemba, Mubele, Bakambu, Kabananga

MOROCCO: Munir, Benatia, Da Costa, Saïss, Dirar, El Ahmadi, Boussoufa, Mendyl, El Kaddouri, Bouhaddouz, Carcela
Tokeo la picha la Hamada Nampiandraza IMAGE
REFA: Hamada Nampiandraza [Madagascar]


AFCON-JAN16A
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment