UGANDA YAFUNDISHWA SOKA NA GHANA.

Tokeo la picha la ayew afcon 2017 image

PENATI YA Dakika ya 30 iliyofungwa na Andre Ayew imewapa Ghana ushindi wa Bao 1-0 walipocheza na Uganda katika Mechi ya Kundi D la AFCON 2017, Mashindano ya 31 ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, iliyochezwa Stade de Port Gentil Mjini Port Gentil Nchini Gabon.
 
Penati hiyo ilitolewa baada ya Isaac Isinde kumvuta Harrison Afful ndani ya Boksi na Andre Ayew, Mchezaji wa Klabu ya West Ham huko England kumfunga Kipa na Mchezaji Bora Afrika Dennis Onyango.

Hii ni mara ya kwanza kwa Uganda kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika tangu 1978 ambazo walifungwa Mechi ya mwisho kabisa, Fainali, na Wenyeji wa Fainali hizo Ghana.
  
Mechi ya Pili ya Kundi D ilichezwa kati ya Mali na Egypt, ambapo timu hizo zilitoshana nguvu kwa kutokufungana.
Leo Jumatano ni Mechi za Pili za Kundi A ambapo Wenyeji Gabon watacheza na Burkina Faso na Vigogo Cameroon kuwavaa wapya wa Mashindano haya Guinea-Bissau.
 
VIKOSI VILIVYOANZA:
GHANA: Braimah Razak, Abdul Rahman Baba [Acheampong 39'], Harrison Afful, Daniel Amartey, John Boye, Mubarak Wakaso, Thomas Teye Partey, Jordan Pierre Ayew [Acquah 85'], Andre Ayew, Christian Atsu, Asamoah Gyan [Badu 72']

UGANDA: Dennis Onyango, Dennis Iguma, Joseph Ochaya, Isaac Isinde [Serunkuma 70'], Hassan Wasswa Mawanda, Tonny Mawejje, Geofrey ‘Baba’ Kizito, Michael Azira [Oloya 45'], Faruku Miya, William Luwaga Kizito [Shaban 57'], Geoffrey Massa.

Tokeo la picha la Joshua Bondo [Botswana] image
Joshua Bondo [Botswana]
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment