JOSE MOURINHO HAACHI MANENO, SOMA ALICHOWAAMBIA LIVERPOOL.

 Tokeo la picha la liverpool vs man u preview image
Jose Mourinho amewaambia mashabiki wake kwamba mechi ya Jumapili dhidi ya Liverpool haitakuwa ''matembezi ya ukumbi wa filamu' na badala yake ameitaka Liverpool kujiandaa vilivyo.

United iliishinda Hull City 2-0 katika awamu ya kwanza ya mechi ya kombe la Ligi EFL siku ya Jumapili kufuatia mabao ya Juan Mata na Marouane Fellaini yaliotikisa wavu.
 Tokeo la picha la clop vs mounriho image

Hata hivyo Mourinho amesema kuwa kila mchezaji anafaa kufanya kazi ya ziada dhidi ya Liverpool.

''Ni mechi muhimu sana kwetu, alisema.Tunapocheza vyema mashabiki pia hushirikiana nasi .

Tunaposhindwa kucheza vizuri ni vyema kwamba mashabiki hawapaswi kulalamika sana.
 Tokeo la picha la liverpool vs man u preview image

Kila mtu anapenda mechi kubwa, wachezaji,wakufunzi na mashabiki. Kila mmoja anapenda mechi kubwa kwa hivyo tuelekee katika mechi hiyo siku ya Jumapili''.

Liverpool imepoteza mara mbili pekee msimu huu ,ikiwa imeshindwa 4-3 na Bournemouth mnamo tarehe 4 mwezi Disemba. 

Timu hiyo ya Jurgen Klopp ni ya pili katika ligi ya Uingereza, ikiwa pointi tano mbele ya United iliopo katika nafasi ya sita na pointi tano nyuma ya viongozi wa ligi Chelsea.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment