YANGA VS MBEYA CITY, KUCHEZWA USIKU.

Tokeo la picha la YANGA VS MBEYA CITY IMAGE
Pambano la Ligi Kuu baina ya Yanga na Mbeya City litachelewa kuanza kwa masaa mawili kinyume na utaratibu wa kawaida wa mechi za Dar kuchezwa kuanzia saa kumi.
Mchezo huo utaanza majira ya saa 12:00 jioni na hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa klabu hiyo kongwe kabisa nchini kucheza mchezo wake wa ligi kuu usiku katika miaka ya hivi karibuni.
Taarifa rasmi ya klabu hio imesema,

“Maamuzi haya yamezingatia matakwa na masilahi ya wadau wa soka nchini ambao wana kiu na hamu ya kuutazama mchezo huo lakini pia wakiwa ni sehemu ya wadau wa mchezo wa riadha itakayofanyika uwanja wa taifa jumamosi hiyo hiyo.
Tunawaomba wanachama na mashabiki wajitokeze kwa wingi kuwapa sapoti vijana wao kwani ulinzi utakuwa imara na thabiti. ”
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment