EFL CUP – NUSU FAINALI: LIVERPOOL CHALI KWA ‘WATAKATIFU’, FAINALI KUWAVAA HULL AU MAN UNITED!

 Southampton's Shane Long scores their first goal
Southampton, maarufu kama 'Watakatifu', imewafunga tena Liverpool 1-0 ndani ya Anfield katika Mechi ya Pili ya Nusu Fainali ya EFL CUP, ambalo ndio Kombe la Ligi huko England, na kutinga Fainali.

Kwenye Mechi ya Kwanza ya Nusu Fainali huko Saint Mary Southampton ilishinda 1-0 kwa Bao la Nathan Redmond na hivyo sasa kutinga Fainali kwa Jumla ya Bao 2-0.
 Liverpool's Loris Karius saves from Southampton's Dusan Tadic

Bao la ushindi la Mechi ya Leo lilifungwa Dakika ya 92 na Shane Long alietokea benchi baada ya kupokea pande zuri kwa kaunta ataki toka kwa Sims ambae nae alitokea benchi.
Southampton's Nathan Redmond in action with Liverpool's James Milner

Leo Usiku, Mechi nyingine ya Marudiano ya Nusu fainali itachezwa huko KCOM Stadium kati Ya Hull City na Manchester United ambao walishinda 2-0 katika Mechi ya Kwanza iliyochezwa Old Trafford.

 Watch Hull City v Manchester United in the second leg of the EFL Cup semi-final live on Sky Sports 1 HD from 7.30pm on Thursday

Mshindi wa Mechi hii atacheza na Southampton ndani ya Wembley Jijini London hapo Februari 26.

 Manchester United beat Hull City 2-0 in the first leg of their EFL Cup semi-final
VIKOSI VILIVYOANZA:

Liverpool: Karius, Alexander-Arnold, Matip, Lovren, Milner, Can, Henderson, Lallana, Firmino, Sturridge, Coutinho.
Akiba: Wijnaldum, Klavan, Moreno, Lucas, Mignolet, Origi, Woodburn.

Southampton: Forster, Cedric, Stephens, Yoshida, Bertrand, Ward-Prowse, Romeu, Davis, Tadic, Rodriguez, Redmond.
Akiba: Clasie, Long, Martina, Hojbjerg, McQueen, Sims, Lewis.
Tokeo la picha la Martin Atkinson IMAGE
Martin Atkinson
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment