EGYPT YAIFUMUA GHANA. RATIBA ROBO FAINALI KUANZA JUMAMOSI.

Tokeo la picha la EGYPT NATIONAL TEAM IMAGE

MECHI za mwisho za Kundi D la AFCON 2017, Mashindano ya 31 ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, zimekamilika Usiku huu huko Gabon na kukamilisha safu ya Mechi za Robo Fainali baada ya Egypt kuilaza Ghana 1-0 na kufuzu na kuungana na hao Ghana waliofuzu kabla ya mechi hiyo.
 
Bao la ushindi ambalo limeiingiza Rgypt Robo Fainali limefungwa Dakika ya 11 na Mohamed Salah.

Katika Mechi nyingine ya Kundi D, Uganda walitangulia kufunga Dakika ya 70 kwa Bao la Farouk Miya na Mali kurudisha Dakika ya 73 kwa Frikiki ya Yves Bissouma.

Robo Fainali zitaanza kuchezwa Jumamosi.

RATIBA YA ROBO FAINALI.

Jumamosi Januari 28
1900 Burkina Faso v Tunisia
2200 Senegal v Cameroon

Jumapili Januari 29
1900 Congo DR v Ghana
2200 Egypt v Morocco 

Nusu Fainali

Jumatano Februari 1
2200 Mshindi RF 1 v Mshindi RF 4

Alhamisi Februari 2
2200 Mshindi RF 2 v Mshindi RF 3

Mshindi wa 3

Jumamosi Februari 4
2200 Aliefungwa NF 1 v Aliefungwa NF 2

Fainali.

Jumapili Februari 5
2200 Finalist 1 v Finalist 2
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment