UEFA CHAMPIONZ LIGI: JUMANNE ARSENAL KUICHAPA BAYERN 4-0 NA KUSONGA?

 Tokeo la picha la UEFA CHAMPIONSHIP IMAGE

Mechi za Pili za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL, zinaanza kuchezwa Jumanne Machi 7 kwa Mechi 2.
 
Siku hiyo, huko Emirates Jijini London, Wenyeji Arsenal wanapaswa kupindua kipigo cha 5-1 walichoshushiwa na Bayern Munich katika Mechi ya Kwanza iliyochezwa huko Germany.

Ili kufuzu kuingia Robo Fainali, Arsenal wanapaswa kitu ambacho hakijawahi kufanyika kwenye UCL kwa kushinda 4-0 ama kwa idadi nyingine ya Mabao ili mradi tofauti ya Magoli iwe 4-0.

Mechi ya Pili ya Jumanne ni huko Naples, Italy wakati Napoli ikirudiana na Mabingwa Watetezi Real Madrid huku wakihitaji ushindi wa Bao 2-0 kwa vile walichapwa 3-1 huko Santiago Bernabeu Jijini Madrid, Spain kwenye Mechi ya Kwanza.

Napoli pia wanaweza kufuzu ikiwa watashinda kwa idadi nyingine ya Mabao ili mradi tofauti ya Magoli iwe 2-0.

Jumatano Machi 8 zipo Mechi nyingine 2 za Pili za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 kati ya Barcelona na Paris Saint Germain huku PSG wakiwa mbele 4-0 na ya pili ni kati ya Borussia Dortmund na Benfica huku Benfica wakiongoza 1-0.

Mechi za Pili za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 zitakamilika Wiki ijayo, Machi 14 na 15, kwa Mechi nyingine 4 ili kutoa Washindi watakaocheza Robo Fainali.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment