ALEXIS SANCHEZ: KUMBE ALIPIGWA BENCHI MECHI NA LIVERPOOL BAADA VURUMAI MAZOEZINI!

   Tokeo la picha la alexis sanchez vs wenger image
IMERIPOTIWA kuwa Alexis Sanchez aligombana na Wachezaji wengine katikati ya Mazoezi yao kuelekea Mechi yao ya Jumamosi waliyotandikwa 3-1 na Liverpool huko Anfield ikiwa ni Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.
 
Imedaiwa Sanchez, Mchezaji kutoka Chile mwenye Miaka 28, alizongwa na wenzake huku mmoja wao akizuiwa ‘kumpiga’.

Baada ya sakata hilo, Meneja wa Arsenal Arsene Wenger hakumuanzisha Sanchez kwenye Mechi na Liverpool akidai ni sababu za kimbinu tu na badala yake kuwatumia Danny Welbeck na Olivier Giroud akieleza kuwa hao ni wazuri kwenye Mipira ya juu akimaanisha Arsenal walitaka kutumia mbinu ya Mipira Mirefu na ya juu kuifyeka Liverpool.

Lakini Wenger akamuingiza Sanchez baada ya Haftaimu na Mchezaji huyo kutoa Pasi kwa Danny Welbeck aliefunga Bao pekee la Arsenal kwenye Mechi hiyo na Liverpool.

Msimu huu, Sanchez ameshiriki kwenye Bao 26 za Arsenal yeye akifunga 17 na kusaidia 9.

Mbali ya vurumai hizo, yapo madai Sanchez hataki kuongeza Mkataba na anataka kuhama mwishoni mwa Msimu huu.

Kipigo hicho cha Liverpool ni cha 3 kwa Arsenal katika Mechi zao 4 za Ligi zilizopita.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment