MASHINDANO
ya 31 ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2017, yameanza Jumamosi
Januari 14 huko Gabon kwa Wenyeji hao kuivaa washiriki wa mara ya kwanza
kabisa Guinea-Bissau na kutoka nao Sare ya 1-1 katika Mechi ya Kundi A.
Bao
la kusawazisha la Guinea Bissau lilifungwa Dakika ya 90 na Juary Soares
wakati Gabon walitangulia kufunga Dakika ya 52 kwa Bao la Supastaa wao
anaecheza Bundesliga huko Germany na Klabu ya Borussia Dortmund
Pierre-Emerick Aubameyang kumalizia Krosi ya Denis Bouanga.
Katika
Mechi nyingine ya Kundi A iliyochezwa Jana, Burkina Faso na Cameroun
nazo zilitoka 1-1 baada ya Cameroon kuongoza kwenye Dakika ya 35 kwa
Frikiki ya Benjamin Moukandjo na Burkinabe kusawzisha Dakika ya 75
kupitia Issoufou Dayo aliemalizia Mpira wa Frikiki uliotemwa Na Kipa
Fabrice Ondoa.
MAKUNDI:
KUNDI A: Gabon, Burkina Faso, Cameroon, Guinea-Bissau
KUNDI B: Algeria, Tunisia, Senegal, Zimbabwe
KUNDI C: Ivory Coast, DR Congo, Morocco, Togo
KUNDI D: Ghana, Mali, Egypt, Uganda
Leo
zipo Mechi 2 za Kundi B wakati Algeria wakicheza na Zimbabwe na
kufuatiwa ile ya Tunisia na Senegal n azote kuchezwa huko Port Gentil
Stadium, Port Gentil, Gabon.
0 Maoni:
Post a Comment