kiungomshambuliaji inakuletea hii; CHELSEA, wakicheza bila Mfungaji wao mkuu Diego Costa, wamepaa Pointi 7 juu kileleni mwa EPL, Ligi Kuu England, baada Jana kuwafunga Mabingwa Watetezi Leicester City 3-0 huko King Power Stadium.
Costa
ambae anadaiwa kufarakana na Timu ya Madaktari wa Viungo wa Timu hiyo
kuhusu madai ya kuumia huku kukiwepo na ripoti za kushinikiza kuhamia China
alitemwa kabisa kwenye Kikosi cha Chelsea cha Mechi hii.
Jana Chelsea ilipiga Bao zake 3 kupitia Marcos Alonso, Bao 2, na Pedro. Usjindi huo umewaweka Chelsea kileleni wakiwa na Pointi 52 kwa Mechi 21 wakifuata Tottenham wenye Pointi 45 kwa Mechi 21.
VIKOSI VILIVYOANZA:
Leicester (Mfumo 3-5-2): Schmeichel; Morgan, Huth, Fuchs; Albrighton, Drinkwater, Ndidi, Mendy, Chilwell; Vardy, Musa
Akiba: King, Kapustka, Simpson, Okazaki, Zieler, Gray, Wasilewski
Chelsea (Mfumo 3-4-3): Courtois; Azpilicueta, David Luiz, Cahill; Moses, Kante, Matic, Alonso; Willian, Hazard, Pedro
Akiba: Begovic, Ivanovic, Fabregas, Zouma, Loftus-Cheek, Batshuayi, Chalobah
Andre Marriner |
0 Maoni:
Post a Comment