Mechi
6 za EPL, Ligi Kuu England, zilizoanza Saa 12 Jioni zimemalizika na
Burnley, Hull City, Stoke City, Arsenal na West Ham kutoka na ushindi
wakati Watford na Middlesbrough zikitoka 0-0.
Burnley
iliichapa Southampton 1-0 kwa Bao la Dakika ya 77 la Joey Barton
aliefunga kwa Frikiki katika Mechi yake ya kwanza tangu ahamie hapo.
Nao
Hull City wameichapa Bournemouth 3-1 kwa Bao 2 za Hernandes na moja la
Mings aliejifunga mwenyewe wakati lile la Bournemouth likifungwa na
Stanislas kwa Penati ya Dakika ya 3 tu.
Sunderland,
wakiwa kwao Stadium of Light, walinyukwa 3-1 na Stoke City waliopata
Bao zao kupitia Marko Arnautovic, Bao 2, na Peter Crouch wakati Jermaine
Defoe aliipa Sunderland Bao lao pekee.
Arsenal,
wakicheza Ugenini, waliichara Swansea City 4-0 kwa Bao za Olivier
Giroud, Alexis Sanchez na 2 walizojifunga wenyewe Swansea kupitia Cork
na Naughton.
West Ham wameitandika Crystal Palace 3-0 kwa Bao za Sofiane Feghouli, Manuel Lanzini na Andy Carroll.
0 Maoni:
Post a Comment