VPL, Ligi Kuu Vodacom, iliendelea jana kwenye Viwanja Viwili na kushuhudia Timu za Nyumbani zote zikishinda 2-0.
Huko
Shinyanga, Stand United imewacharaza wenzao wa Mkoa huo Mwadui FC Bao
2-0 kwa Bao za Jacob Massawe na Adeyum Salehe na kujikita Nafasi ya 6
wakati Mwadui wapo wa 10.
Huko Kaitaba Mjini Bukoba, Kagera Suga imeifunga Ndanda FC 2-0 kwa Mabao ya Mbaraka Yusuph aliefunga zote.
Ushindi huu umewaweka Kagera Sugar Nafasi ya 3 wakati Ndanda FC wakiwa wa 13.VPL inaendelea Jumapili hii kwa Mechi 1 huko CCM Kirumba, Mwanza kati ya Mbao FC na African Lyon.
0 Maoni:
Post a Comment