KEITH
HACKETT, Refa na Mkuu wa zamani wa PGMOL (Professional Game Match
Officials Limited), Kampuni inayosimamia Marefa wa EPL, Ligi Kuu
England, ameungana na Jose Mourinho kwenye msimamo kuwa Meneja huyo wa
Manchester United hatendewi haki na Marefa.
Hackett
amebainisha kuwa Sheria hutafsiriwa tofauti kwa Mourinho ukilinganisha
na Mameneja wengine na adhabu anazopewa pia huwa tofauti na wengine.
Hackett
amenyooshea kidole adhabu ya Wenger ya kufungiwa Mechi 4 kutokaa Benchi
kwa kumsukuma Refa wa Akiba wakati Mourinho alifungiwa kutokanyaga
kabisa Uwanjani kwa kumpandishia tu Refa.
KEITH HACKETT |
Hackett
pia alisema kitendo alichofanya Jurgen Klopp cha kumtolea ukali Refa wa
Akiba Majuzi wakati Timu yake ikitoka 1-1 na Chelsea huko Anfield na
kutofanywa chochote angekuwa Mourinho angetolewa nje na kufuata Kifungo
juu.
Hackett amesema kutofuatwa Sheria kikamilifu na kutumika kufuatana na nani Mkosaji kunaleta dhuluma ya haki.
Majuzi,
Meneja wa Man United Jose Mourinho alilalamika na kudai yeye anaamuliwa
kwa Sheria tofauti ukilinganisha na Mameneja wengine wa EPL.
Akiongea
baada ya Mechi na Hull City, Mourinho alichukizwa na Refa Mike Jones
kwa kushindwa kuwadhibiti Hull waliokuwa wakipoteza muda mno ili kulinda
Sare yao na Mreno huyo kuongea na Refa wa Akiba.
Mourinho ameeleza: "Mnajua wazi mie niko tofauti. Sheria kwangu zipo tofauti."
Aliongeza:
"Jana Refa wa Akiba alimwambia Meneja: 'Nafurahia sana msisimko wako'.
Leo mie naambiwa kaa chini au tutakutoa Uwanjani!"
Msimu
huu tayari Mourinho ameshatwangwa Vifungo Viwili kutokana na kuongea
kuhusu Refa na pia kupiga Teke Chupa ya Maji akiwa Uwanjani.
0 Maoni:
Post a Comment