COPA DEL REY: BARCA YATINGA NUSU FAINALI KWA KISHINDO.

Picha inayohusiana

MABINGWA Watetezi wa Kombe la Mfalme wa huko Spain, Copa del Rey, FC Barcelona, Jana waliitandika Real Sociedad Bao 5-2 kwenye Mechi ya Pili ya Robo Fainali.
 
Kwenye Mechi ya Kwanza iliyochezwa huko Anoeta Stadium, Barca ilishinda 1-0 na hivyo sasa wametinga Nusu Fainali kwa Jumla ya Mabao 6-2.

 Tokeo la picha la BARCA VS REAL SOCIEDAD COPA DEL REY IMAGE

Hapo Jana, Bao za Barca zilifungwa na Denis Suarez, Bao 2, Lionel Messi, Penati, Luis Suarez na Arda Turan.

Bao za Real Sociedad zilipachikwa na Juanmi na Da Silva.
Kwenye Nusu Fainali, Barcelona, ambao wametwaa Copa Del Rey mara 28, wataungana na Atletico Madrid, Celta Vigo na Alaves.

Droo ya Nusu Fainali itafanyika baadae Leo
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment