TRAIKA Diego Costa ametupwa nje ya Kikosi cha Chelsea ambacho Leo kipo huko King Power Stadium kucheza na Mabingwa Watetezi Leicester City katika Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.
Habari
za ndani zimedai upo mzozo wa Costa, mwenye Miaka 28, na uongozi wa
Klabu akisindikiza ahamie China kwa Dau la Pauni Milioni 30.
Hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la Wachezaji Wakubwa Duniani kutua huko China ambako wanalipwa Mishahara minono mno.
Wiki
yote hii, Costa amekuwa hayupo Mazoezini akidai ameumia na pia kuzozana
na Madktari wa Viungo wa Chelsea mzozo ambao umesemekana ulimhusisha pia
Meneja Antonio Conte.
Hivi sasa ripoti zimedai Wakala wa Conte, Jorge Mendes, yupo huko China. Kikosi cha Chelsea ambacho Jana kilijumuika pamoja kuelekea huko Leicester kiliondoka bila Costa.
Hata
hivyo, msimamo wa Chelsea ni kwamba hawatamuuza Mchezaji huyo Mzaliwa
wa Brazil anaechezea Spain na watabaki nae hadi mwisho wa Mkataba wake
hapo 2019.
Msimu
huu, Costa ameifungia Chelsea Bao 14 na kuasisti mara 5 huku Chelsea
ikiongoza EPL ikiwa Pointi 5 juu kileleni mbele ya Timu ya Pili
Liverpool.
0 Maoni:
Post a Comment