HIMID
MAO amepeleka Kombe la Mapinduzi ambayo ni Mashindano ya kuenzi Miaka
53 ya Mapinduzi Tukufu ya Visiwa vya Zanzibar na Pemba, kwa Bao lake
pekee wakati Azam FC ikifunga Simba 1-0 Uwanjani Amaan Stadium huko
Zanzibar Jana Usiku.
Mao alifunga Bao hilo Dakika ya 13 kwa Shuti kali la Mita 25 ambalo Kipa wa Simba Daniel Agyei hakuona ndani.
Baada
ya Mechi hiyo Nahodha wa Azam FC, John Bocco, alikabidhiwa Kombe la
Mapinduzi na Rais wa Zanzibar, Dokta Ali Mohammed Shein.
Simba
walitinga Fainali hii kwa mbwembwe kubwa baada ya kuwabwaga Watani zao
Yanga kwa Mikwaju ya Penati 4-2 na Washabiki wao wengi waliamini hilo
liliwafanya wastahili Kombe la kini Azam FC, wakiwa chini ya Kocha wa
muda, Idd Cheche, walikuwa na stori nyingine kabisa.
Sasa
Timu hizi zote zinarejea Bara kucheza VPL, Ligi Kuu Vidacom, ambapo
Simba watakuwa dimbani Jumatano huko Jamhuri, Morogoro kuivaa Mtibwa
Sugar na Siku hiyo hiyo Azam FC kuwa kwao Chamazi kucheza na Mbeya City.
VIKOSI VILIVYOANZA:
AZAM FC:
Aishi Manula, Shomari Kapombe, Gardiel Michael, Aggrey Moris, Yakubu
Mohammed, Stephan Mpondo, Joseph Mahundi, Salum Abubakar, John Bocco,
Yahya Mohammed, Himid Mao.
SIMBA:
Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein, Abdi Banda, Method
Mwanjali, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, James Kotei, Juma Luizio, Muzamiru
Yassin, Mwinyi Kazimoto
0 Maoni:
Post a Comment