LA LIGA: JUMAPILI REAL KUIVAA REAL SOCIEDAD.

Tokeo la picha la real madrid image

VINARA wa La Liga huko Spain Real Madrid Jumapili watakuwa Wenyeji wa Timu ngumu Real Sociedad na sasa wapo kwenye kibarua kigumu cha kugeuza fomu yao iliyoporomoka ambayo imewafanya washindwe kushinda katika Mechi zao 3 kati ya 4 zilizopita.
 
Katikati ya Wiki, Real walibwagwa nje ya Copa del Rey walipotoka 2-2 na Celta Vigo baada ya kufungwa Mechi ya Kwanza 2-1.

Hata hivyo, kwenye La Liga, Real, chini ya Kocha Zinedine Zidane, wapo Pointi 1 mbele ya Sevilla na 2 mbele ya Barcelona huku wao wakiwa wamecheza Mechi 1 pungufu.

Kuporomoka kwa fomu ya Real kumeandamwa na kuwa na Majeruhi 7 kwenye Kikosi chao cha Kwanza ambao ni Raphael Varane, Gareth Bale, James Rodriguez, Luka Modric, Marcelo, Dani Carvajal na Pepe ingawa Varane huenda akacheza Mechi na Sociedad.

Nao Real Sociedad watatinga kwenye Mechi hii na Real huko Santiago Bernabeu wakitoka kwenye kichapo cha 5-2 toka kwa Barcelona kwenye Mechi ya Copa del Rey.

Jumapili Barcelona watacheza Mechi yao mapema Ugenini na Real Betis na ushindi kwao utawafanya waongoze La Liga kwa muda kwa vile Real na Sevilla watacheza Mechi zao baadae.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment