MAN CITY YACHAKAZWA BILA HURUMA NA EVERTON.

Tokeo la picha la everton vs man city image

EVERTON jana huko Goodison Park imewaonyesha Manchester City kwamba wao wapo juu kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, kwa kuwatandika Bao 4-0 kipigo ambacho ni kibaya mno kwa Meneja wa City katika himaya yake kwenye Mechi za Ligi.
 
City walikuwa nyuma 1-0 hadi Haftaimu kwa Bao la Romelu Lukaku la Dakika ya 34.
 Tokeo la picha la lukaku image

Kipindi cha Pili Everton wakatandika Bao nyingine 3 katika Dakika 47, 79 na 90 Wafungaji wakiwa Kevin Mirallas na Chipukizi Tom Davies na Ademola Lookman.
 Tokeo la picha la Tom Davies image

Matokeo hayo yamewaacha City wakiwa Nafasi ya 5 na Everton wakiwa Nafasi ya 7.

Mechi inayofuata kwa City ni Jumamosi ijayo wakiwa kwao Etihad kucheza na Timu ngumu Tottenham Hotspur wakati Everton wako Ugenini huko Selhurst Park kucheza na Crystal Palace.

VIKOSI VILIVYOANZA:

EVERTON: Robles, Holgate, Ashley Williams, Funes Mori, Coleman, Davies, Barry, Baines, Barkley, Mirallas, Lukaku
Akiba: Schneiderlin, Jagielka, Lennon, McCarthy, Valencia, Stekelenburg, Lookman. 

MAN CITY: Bravo, Sagna, Otamendi, Stones, Clichy, Zabaleta, Touré, Silva, De Bruyne, Sterling, Agüero
Akiba: Kolarov, Caballero, Jesus Navas, Delph, Sané, Iheanacho, García. 
Tokeo la picha la Mark Clattenburg image
Mark Clattenburg.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment