MAN U KINARA WA MAPATO KWA VILABU DUNIANI.

hii ni kwa mara ya kwanza Man U kuongoza tokea mwaka 2004
Hii ni kwa mara ya kwanza Man U kuongoza tokea mwaka 2004

Timu ya Manchester United imepata kipato kikubwa kuliko timu yoyote katika msimu uliopita kulingana na taarifa zilizochapishwa na kampuni kubwa ya ukaguzi duniani (Deloitte).
Manchester United imewashinda Real Madrid waliofanya vizuri katika michezo kwa miaka 11baaada ya kukusanya kipato kikubwa takribani Euro 689 katika msimu wa 2015-2016.
Clubu za ligi ya Premier imeshuhudia kukua kwa kipato kwa Euro Millioni mia moja.

Mauzo makubwa ya jezi ni moja ya chanzo cha mapato kwa United
Mauzo makubwa ya jezi ni moja ya chanzo cha mapato kwa United
Ukijumlisha vipato vya timu ishirini bora kwa msimu wa 2015-2016 vimeongezeka kwa asilimia 12% na kufikia euro billioni 7.4 hii haijawahi kutokea.

Hii ni mara ya kwanza kwa Man U kushikilia nafasi hiyo tokea msimu wa 2003-04.
Picha inayohusiana
Barcelona inasalia nafasi ya pili
Real Madrid wameshuka mpaka nafasi ya tatu wakiwaacha wapinzani wao wakubwa Barcelona katika nafasi ya pili.

Picha inayohusiana
Madrid imeshuka mpaka nafasi ya tatu
Mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich wapo nafasi ya nne huku matajiri wa jiji la Manchester Man City wakiwa nafasi ya tano kwa kutengeneza Euro milioni524 kwa msimu uliopita.

Hii ni mara ya kwanza kwa city kuingia katika nafasi hiyo.

Msimamo kwa Mapato Orodha ya Deloitte 2015-16 KUMI BORA
Klabu (Nafasi msimu uliopita)         Mapato kwa €m (£m kwenye mabanos) 2015-16    Mapato 2014-15
1 (3) Manchester United        689 (515.3)    519.5 (395.2)
2 (2) Barcelona        620.2 (463.8)    560.8 (426.6)
3 (1) Real Madrid        620.1 (463.8)    577 (439)
4 (5) Bayern Munich        592 (442.7)    474 (360.6)
5 (6) Manchester City        524.9 (392.6)    463.5 (352.6)
6 (4) Paris St-Germain        520.9 (389.6)    480.8 (365.8)
7 (7) Arsenal        468.5 (350.4)    435.5 (331.3)
8 (8) Chelsea        447.4 (334.6)    420 (319.5)
9 (9) Liverpool        403.8 (302)    391.8 (298.1)
10 (10) Juventus        341.1 (255.1)    323.9 (246.4)
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment