MANCHESTER UNITED YAZIDI KUNG'AA EFL

Tokeo la picha la MAN U VS HULL CITY IMAGE EFL
Manchester United, ikiongozwa na Meneja Jose Mourinho, wamepiga hatua kubwa kuelekea kutwaa Taji kubwa la pili Msimu huu baada ya Jana huko kwao Old Trafford kuichapa Hull City 2-0 katika Mechi ya Kwanza ya Nusu Fainali ya EFL CUP, ambalo ndio Kombe la Ligi huko England.

Mwanzoni mwa Msimu, Man United walitwaa Ngao ya Jamii.

Bao za Man United, waliochezesha karibu Kikosi chao chote, zilifungwa na Juan Mata na Marouane Fellaini alieanzia Benchi.

Bao la Mata lilifungwa Dakika ya 56 alipounganisha Kichwa cha Henrikh Mkhitaryan na la pili Dakika ya 87 kupitia Fellaini alieunganisha Krosi ya Matteo Darmian.
Hull City na Man United zitarudiana huko KCOM Stadium hapo Januari 28.
Tokeo la picha la MAN U VS HULL CITY IMAGE EFL
Leo Jumatano Januari 11 itachezwa Nusu Fainali ya Pili huko Saint Mary kwa Southampton kucheza na Liverpool.

Nusu Fainali hizi huchezwa kwa Mikondo Miwili ya Nyumbani na Ugenini na hivyo Marudiano ya Mechi hizi yatakuwa hapo Januari 25 na 26 huko Anfield na KCOM Stadium.

 EFL CUP
Nusu Fainali.

Ratiba/Matokeo:

Jumanne Januari 10
Manchester United 2 Hull City 0

Jumatano Januari 11
**Saa za Bongo
2245 Southampton V Liverpool

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment