ROONEY APONGEZWA NA AITWA LEGENDARY.

 Tokeo la picha la rooney image
Sir Bobby Charlton, ambae kwa muda mrefu alishikilia Rekodi ya kufunga Bao nyingi Klabuni Manchester United hadi Juzi ilipovunjwa na Wayne Rooney, amemsifia Straika huyo na kumsema ni 'Lejendari wa kweli kwa Klabu na Nchi yake'.
 
Wakiwa nyuma kwa Bao 1-0 walipocheza na Stoke City Ugenini kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, Rooney aliisawazishia Man United kwa Frikiki ya Dakika ya 94 na kufikisha Bao 250 akiivunja Rekodi ya Sir Bobby Charlton aliefunga Bao 249 iliyodumu kwa Miaka 44.
 Tokeo la picha la sir bobby charlton image
 
Sir Bobby Charlton alikuwepo kwenye Mechi hiyo ambapo mwishoni alikwenda Vyumba vya Kubadili Jezi kumpongeza Rooney.
 
Akiongea baadae, Sir Bobby alisema: "Nitakuwa mwongo nikisema sikuhuzunika kuipoteza hii rekodi. Lakini ukweli nimefurahishwa na Wayne. Anastahili mahala kwenye Vitabu vya Historia. Yeye ni Lejendari wa kweli wa Klabu na Nchi yake na ni sahihi yeye kuwa ndie Mfungaji Bora kwa Man United na England!"
 
 Tokeo la picha la sir alex furguson image
 
Nae Sir Alex Ferguson, aliekuwa Meneja wa Man United kuanzia 1986 hadi 2013 na Agosti 2004 kumnunua Rooney kutoka Everton, amesema: "Nampa pongezi kubwa Wayne kwa rekodi hii. Wayne anastahili kuwemo kwenye Historia wa Klabu hii kubwa na nina hakika atafunga Bao nyingi zaidi.
 Tokeo la picha la jose morinho image
Meneja wa sasa wa Man United, Jose Mourinho, ameeleza:: "Ni rekodi ya Klabu kubwa kabisa England na moja ya Klabu kubwa Duniani. Kabla ya hapo rekodi hiyo ilishikiliwa na Lejendari wa Klabu. Sasa Wayne anakuwa Lejendari wa Manchester United."
 
Rooney, mwenye Miaka 31, amesema: "Naskia fahari sana. Hakikuwa ni kitu nilichokitegemea nilipojiunga! Wachezaji wanaochezea Klabu hii ni kiwango cha Dunia. Nasikia fahari kuichezea Klabu hii na kuwa ndie Mfungaji Bora katika Historia yake ni tuzo kubwa mno!"
 Tokeo la picha la Gareth Southgate image
Nae Meneja wa England Gareth Southgate, akiongea na Tovuti ya FA, Chama cha Soka England, ametamka: "Ukiangalia ni Rekodi ya nani ameivunja na jinsi ambavyo Sir Bobby anavyopendwa na Nchi na Klabu yake inaonyesha wazi hii ni sifa kubwa. Kuwa Mfungaji Bora kwa Man United na pia England ni mafanikio makubwa mno! Kufunga Bao zote hizo kunataka uwe Mchezaji mzuri kwa kipindi kirefu!"
 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment