ALEXIS SANCHEZ AIPELEKA ARSENAL NAFASI YA PILI EPL

 Alexis v Burnley
Arsenal wakiwa kwao Emirates wamefanikiwa kushinda 2-1 kwa Penati Dakika za Majeruhi wakati wakiwa Mtu 10 na pia kumpoteza Meneja wao Arsene Wenger alietolewa nje ya Uwanja na Refa.
 
Ushindi huo umewaweka Arsenal Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 9 nyuma ya Vinara Chelsea.


Arsenal walitangulia kufunga Dakika ya 59 kwa Bao la Sentahafu wao Mustafi lakini Dakika ya 65 wakabaki Mtu 10 baada Kiungo wao Xhaka kupewa Kadi Nyekundu.

Burnley walisawazisha kwa Penati ya Dakika za Majeruhi zilizoongezwa 7 kupitia Gray katika Dakika ya 93 baada ya Refa Jon Moss kuamua Francis Coquelin alimchezea Faulo Ashley Barnes na Andre Gray kusawazisha.

Tukio hilo lilimfanya Wenger alalamike sana na Refa Moss kumtimua Uwanjani.

Lakini Refa huyo, katika Dakika ya 98, aliwapa Arsenal Penati baada kuamua Buti ya Ben Mee ilikuwa juu Kichani mwa Laurent Koscielny na Alexis Sanchez kufunga Bao la Pili na la ushindi kwa Arsenal.

Mapema Jana, Southampton wakiwa kwao Saint Mary, waliwatandika Mabingwa Watetezi Leicester City 3-0 kwa Bao za Ward-Prowse, Rodriguez na Penati ya Tadic na kuwaacha Mabingwa hao wakiwa wameenda Gemu 11 za Ugenini kwenye EPL Msimu huu bila ushindi.

Sasa Leicester wapo Nafasi 3 juu ya zile Timu 3 za mkiani huku Southampton wakipanda hadi Nafasi ya 11.

Ligi Kuu England Ratiba
++Saa za Bongo++

[Zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku isipokuwa inapotajwa]

Jumanne Januari 31
Arsenal v Watford            
Bournemouth v Crystal Palace               
Burnley v Leicester City              
Middlesbrough v West Bromwich Albion          
Sunderland v Tottenham Hotspur          
Swansea City v Southampton               
2300 Liverpool v Chelsea   
         
Jumatano Februari 1
West Ham United v Manchester City               
2300 Manchester United v Hull City                
2300 Stoke City v Everton  

Jumamosi Februari 4
1530 Chelsea v Arsenal               
1800 Crystal Palace v Sunderland          
1800 Everton v Bournemouth               
1800 Hull City v Liverpool           
1800 Southampton v West Ham United           
1800 Watford v Burnley              
1800 West Bromwich Albion v Stoke City         
2030 Tottenham Hotspur v Middlesbrough  
              
Jumapili Februari 5
1630 Manchester City v Swansea City             
1900 Leicester City v Manchester United          
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment