SERGIO RAMOS AWA SHUJAA, HUKU RONALDO AKIZOMEWA UWANJANI.

 Tokeo la picha la sergio ramos image

JANA Nahodha wa Real Madrid ambao ni Vinara wa La Liga Sergio Ramos alifunga Bao 2 wakati Timu yake ikiichapa 2-1 Malaga huko Santiago Bernabeu kwenye Mechi ya Ligi ambayo Nyota wa Real Cristiano Ronaldo akizomewa na baadhi ya Mashabiki wa Timu hiyo.
 
Baada ya Mechi 18 kwa kila Timu Real wanaongoza La Liga wakiwa na Pointi 43 wakifuatiwa na Sevilla wenye 39, Barcelona 38 na kisha Atletico Madrid wenye 34.
 
Jana Ramos alifunga Bao la Kwanza Dakika ya 35 kwa Kichwa kufuatia Kona ya Toni Kroos na kisha kupiga la pili Dakika ya 43 huku Malaga wakifunga Bao lao moja Dakika ya 63 kupitia Juanpi Anor.
 
Kwenye Mechi hiyo Ronaldo alikosa nafasi kadhaa zilizookolewa na Kipa Kameni na moja kupiga Posti kitu ambacho kiliwachukiza Mashabiki ambao baadhi yao walimzomea.
 Tokeo la picha la CHRISTIANO RONALDO IMAGE
 
Kitu hicho kilimsikitisha Meneja wa Real Zinedine Zidane ambae aliwaasa Mashabiki hao kuwapa moyo Wachezaji.
 
Leo Timu za Pili na za 3, Sevilla na Barca, zipo Ugenini kucheza Mechi zao za La Liga.
 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment