ASAMOAH GYAN AIPELEKA GHANA ROBO FAINALI, UGANDA ASANTENI KWA KUSHIRIKI NA KARIBUNI NYUMBANI.

Tokeo la picha la Asamoah Gyan afcon 2017 image

WAKATI Asamoah Gyan akiifungia Ghana Bao pekee walipoifunga Mali 1-0 huko Gabon katika Mechi ya Pili ya Kundi D la AFCON 2017, Egypt, katika Mechi nyingine ya Kundi D, waliifunga Uganda 1-0 na kuwatupa nje Uganda katika Mashindano hayo.
 
Mapema Jana huko Port-Gentil, Gyan alifunga Bao pekee na kuifanya Ghana wawe Nchi ya Pili kutinga Robo Fainali baada ya Juzi Senegal nao kusonga wakibakisha Mechi 1 katika Makundi yao.
 Tokeo la picha la uganda national team image
 
Katika Mechi ya Pili ya Kundi D, Bao la Dakika ya 89 la Mchezaji alieanzia Benchi Abdallah El Said liliipa ushindi Egypt wa 1-0 na kuitupa Uganda nje ya Nashindano huku wakibakisha Mechi 1.
 
Katika Mechi ya mwisho, Ghana watacheza na Egypt hapa Jumatano na Egypt wanahitaji Sare tu ili kufuzu.
Siku hiyohiyo Mali watahitaji kuifunga Uganda Siku hiyo ya Jumatano huku wakiomba Egypt ifungwe ili wao wafuzu 
 
Leo Jumapili zipo Mechi za mwisho za Kundi A huko Libreville ambapo Wenyeji Gabon watalazimika kuifunga Cameroon ili kufuzu na Sare itawaacha waombe matokeo mema kwao katika Mechi nyingine ya Kundi hilo kati ya Burkina Faso na Guinea-Bissau.
 
Jana Rais wa Gabon Ali Bongo aliwatembelea Wachezaji wa Nchi hiyo ili kuwapa morali
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment