CITY, SPURS SARE, LIVERPOOL WACHEZEA KICHAPO NYUMBANI.

 Tokeo la picha la DELE ALLI IMAGE
MAN CITY na Tottenham Hotspur Jana zilitoka Sare 2-2 huko Etihad Jijini Manchester katika Mechi ya EPL, Ligi Kuu England.
 
City walitangulia kufunga katika Dakika za 49 na 54 kupitia Leroy Sane na Kevin De Bruyne na Spurs kusawazisha Dakika za 58 na 77 kwa Bao za Dele Alli na Son Heung-min.
 Tokeo la picha la Leroy Sane na Kevin De Bruyne IMAGE

Mchezaji Mpya wa City kutoka Brazil, aliingizwa mwishoni kutoka Benchi na kufunga lakini Bao hilo lilikataliwa kwa kuwa Ofsaidi.

Matokeo hayo yamewaacha City Nafasi ya 5 huku Spurs wapo Nafasi ya Pili.

Mapema hiyo hiyo Jana huko Anfield, Liverpool walichapwa 3-2 na Swansea City katika Mechi nyingine ya EPL.

Bao za Liverpool zilipachikwa Dakika za 56 na 69 na Firmino wakati Swansea walifunga Dakika za 48 na 52 kwa Bao za Llorente na 74 la Gylfi Sigurdsson.

Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment