WASHIKA BUNDUKI "ARSENAL" WAPIGWA NA BUNDUKI ZAO EMIRATES STADIUM.

Mara ya mwisho Watford kuifunga Arsenal katika uwanja wake wa nyumbani ilikuwa 1988
Mara ya mwisho Watford kuifunga Arsenal katika uwanja wake wa nyumbani ilikuwa 1988

Matumaini ya klabu ya Arsenal kutwaa ubingwa wa England yanaanza kufifia baada ya kuchapwa na Watford 2-1 na hii ni Emirates.

Mlinzi wa zamani wa Tottenham Younes Kaboul alianza kuiandikia Watford goli la kwanza dakika ya 10 baada ya kuachia shuti kali lililomgonga Aaron Ramsey na kutinga nyavuni.

Dakika mbili na sekunde 57 baadaye Troy Deeney akaiandikia goli la pili Watford baada ya mpira uliopigwa na Etienne Capoue kupanguliwa na mlinda mlango Peter Cech na kisha kumkuta Troy aliyendika bao safi.

Kipindi cha pili Arsenal walianza kwa kasi na kujipatia goli la kufutia machozi kutoka kwa Alex Iwobi baada ya kupata pande safi lililochongwa na Alexis Sanchez.

Kwa mara ya mwisho Arsenal kushinda kikombe cha ligi kuu England ilikuwa msimu wa mwaka 2003-04 na kwa sasa wapo nyuma kwa alama tisa dhidi ya vinara Chelsea ambao wametoka suluhu ya 1-1 dhidi ya Liverpool.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment