BAADA YA KUFUKUZWA LEICESTER, RANIERI ANENA: ‘JANA NDOTO YANGU ILIKUFA!’

 Tokeo la picha la claudio ranieri image

CLAUDIO Ranieri, Meneja alieipa Leicester City Ubingwa wao wa kwanza katika Historia yao na kufukuzwa kazi baada ya Miezi 9 tu, Leo ametoa tamko ambalo limechoma Mioyo ya wengi.
 
Alianza: ‘Jana Ndoto yangu ilikufa!’
 RANIERI-NDOTO
















AWALI:
MABINGWA wa England LeicesterCity wamemfukuza kazi Meneja wao ikiwa ni Miezi 9 tu baada ya kuwapa, bila kutegemewa, Ubingwa wao wa kwanza wa England katika Historia yao.

Habari hizi zimetolewa na Bodi ya Leicester City na zimekuja Siku 1 tu baada ya Klabu hiyo kufungwa 2-1 huko Spain na Sevilla katika Mechi yao ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.

Ranieri, mwenye Miaka 65, aliiongoza Leicester, kwa mshangao wa wengi, kutwaa Ubingwa wa England Msimu uliopita wakiwa mbele kwa Pointi 10 lakini Msimu huu mambo yako mrama na wako hatarini kuporomoka Daraja.

Likitokea hilo basi wao ndio watakuwa Mabingwa Watetezi wa kwanza wa England kushuka Daraja tangu 1938.

Leicester wamepoteza Mechi zao 5 za Ligi zilizopita na ndio Klabu pekee katika Madaraja yote Manne ya England ambayo haijafunga hata Bao 1 la Ligi Mwaka huu 2017.

Mechi ijayo kwa Leicester ni kwao King Power Stadium Jumatatu ijayo dhidi ya Liverpool.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment