CLAUDIO RANIERI AFUKUZWA LEICESTER CITY, MIEZI 9 TU BAADA YA KUWAPA UBINGWA ENGLAND.

 Tokeo la picha la CLAUDIO RANIERI IMAGE

MABINGWAwa England LeicesterCity wamemfukuza kazi Meneja wao ikiwa ni Miezi 9 tu baada ya kuwapa, bila kutegemewa, Ubingwa wao wa kwanza wa England katika Historia yao.


Habari hizi zimetolewa na Bodi ya Leicester City na zimekuja Siku 1 tu baada ya Klabu hiyo kufungwa 2-1 huko Spain na Sevilla katika Mechi yao ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.

    Tokeo la picha la CLAUDIO RANIERI IMAGE
Ranieri, mwenye Miaka 65, aliiongoza Leicester, kwa mshangao wa wengi, kutwaa Ubingwa wa England Msimu uliopita wakiwa mbele kwa Pointi 10 lakini Msimu huu mambo yako mrama na wako hatarini kuporomoka Daraja.

Likitokea hilo basi wao ndio watakuwa Mabingwa Watetezi wa kwanza wa England kushuka Daraja tangu 1938.

Leicester wamepoteza Mechi zao 5 za Ligi zilizopita na ndio Klabu pekee katika Madaraja yote Manne ya England ambayo haijafunga hata Bao 1 la Ligi Mwaka huu 2017.

Mechi ijayo kwa Leicester ni kwao King Power Stadium Jumatatu ijayo dhidi ya Liverpool.

Jumamosi Februari 25
1800 Chelsea v Swansea City               
1800 Crystal Palace v Middlesbrough              
1800 Everton v Sunderland         
1800 Hull City v Burnley             
Southampton v Arsenal [IMEAHIRISHWA]
1800 West Bromwich Albion v Bournemouth              
2030 Watford v West Ham United 
        
Jumapili Februari 26
1630 Tottenham Hotspur v Stoke City             
Manchester City v Manchester United [IMEAHIRISHWA]

Jumatatu Februari 27
2300 Leicester City v Liverpool
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment