EFL: MANCHESTER UNITED YAWA BINGWA, HUKU IBRAHIMOVIC AKING'AA.

Manchester United waliilaza Souythampton mabao 2-1 ili kushinda kombe la EFL
Mshambuliaji wa Manchesater United Zlatan Ibrahimovic alifunga bao la ushindi dakika za mwisho na kumpatia mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho kombe lake la kwanza tangu ajiunge na klabu hiyo kwa kuishinda Southampton.
Southampton walionyesha mchezo mzuri wakati wa mechi hiyo lakini wakavunjwa moyo na uamuzi wa utata uliompa bao la ushindi raia huyo wa Sweden mwenye umri wa miaka 35.
Wachezaji wa Southampton wakisherehekea bao la Manolo GabbiadianiHaki miliki ya pichaREX FEATURES
Image captionWachezaji wa Southampton wakisherehekea bao la Manolo Gabbiadiani
Mshambuliaji wa Saints Manolo Gabbiadiani alifunga bao lililokataliwa kabla ya Manchester United kupata bao la pili kupitia Ibrahimovic kunako dakika 19 kabla ya Jesse Lingard kufunga ikiwa imesalia dakika saba mechi kukamilika.
Southampton ilifunga mabao yake mawili kupitia Gabbiadiani katika vipindi vyote viwili vya mechi.
Zlatan IbrahimovicHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionZlatan Ibrahimovic
Oriel Romeu alipiga mwamba wa goli kabla ya Ibrahimovic kufunga kupitia krosi iliopigwa na Anders Herrea dakika tatu kabla ya mechi kukamilika na hivyobasi kuipatia ushindi Manchester United.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment