WAKATI
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger akiwa Jukwaani miongoni mwa Mashabiki
wa Chelsea kushuhudia Arsenal ikiwavaa Vinara wa EPL, Ligi Kuu England,
Chelsea, Meneja wao Antonio Conte ameitaka Timu yake kutumia nafasi hii
murua kupiga hatua kuelekea Ubingwa.
Wenger
haruhusiwi kukaa Benchi la Ufundi la Timu yake kwa vile yupo Kifungoni
na alipaswa kukaa Jukwaa la Wakurugenzi lakini muundo wa Stamford Bridge
ni tofauti na akikaa huko atakuwa mbali na Benchi la Ufundi kwa vile
liko upande wa pili wa Uwanja.
Ili kuwa karibu na Benchi, Wenger atalazimika kukaa pamoja na Washabiki wa Chelsea akiwekewa ulinzi mkali.
Kifungo cha Wenger hakimzuii kutoa maelekezo wakati wa Mechi.
Hivi
sasa Chelsea wanaongoza EPL wakiwa Pointi 9 mbele huku Gemu zikibaki 15
na wakiifunga Arsenal, Timu ambayo iliifunga Chelsea 3-0 kwenye Mechi
yao ya kwanza ya Ligi Msimu huu huko Emirates.
Kipigo hicho kiliibadilisha Chelsea na Conte akaja na Mfumo mpya wa 3-4-3 wakicheza Mechi 17 za Ligo na kufungwa 1 tu.
Pia vita nyingine katika mechi hii ni kati ya DIEGO COSTA NA ALEXIS SANCHEZ katika kugombania nafasi ya kuongoza katika ufungaji bora wa EPL.
Pia vita nyingine katika mechi hii ni kati ya DIEGO COSTA NA ALEXIS SANCHEZ katika kugombania nafasi ya kuongoza katika ufungaji bora wa EPL.
Conte
ameeleza: "Zipo 15 zimebaki na ni Pointi 45. Wao ni Timu nzuri
inayoweza kupigania Ubingwa na usisahau kwao walitufunga 3-0!"
Aliongeza: "Lakini hii ni nafasi nzuri kwetu na sisi ni Timu tofauti.
Wakati
Chelsea wanatinga Mechi hii wakitokea Anfield ambako Jumanne walitoka
1-1 na Liverpool, Arsenal wanatoka kwao Emirates walikodundwa 2-1 na
Watford.
Hii ni Mechi ngumu kwa Arsenal kwani hawajashinda hapo Stamford Bridge tangu 2011.
Kipa
wa Arsenal Petr Cech, ambae kabla alidakia Chelsea na kutwaa nao
Ubingwa mara 4, ameelezea kipigo cha Watford ni pigo kubwa katika azma
yao ya Ubingwa na kuitaka Timu yao kukaza Buti.
EPL – Ligi Kuu England Ratiba
***Saa za Bongo***
Jumamosi Februari 4
1530 Chelsea v Arsenal
1800 Crystal Palace v Sunderland
1800 Everton v Bournemouth
1800 Hull City v Liverpool
1800 Southampton v West Ham United
1800 Watford v Burnley
1800 West Bromwich Albion v Stoke City
2030 Tottenham Hotspur v Middlesbrough
Jumapili Februari 5
1630 Manchester City v Swansea City
1900 Leicester City v Manchester United
0 Maoni:
Post a Comment