VPL: KIKOSI CHA YANGA CHAREJEA MAZOEZINI, BAADA YA MAPUMZIKO MAFUPI.



Kikosi cha Yanga kinarejea uwanjani leo kuanza maandalizi ya mechi yake ya mwisho ya Ligi Kuu Bara.

Wachezaj hao watarejea mazoezini leo na kuanza kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Taifa, hii ikiwa ni baada ya mapumziko ya siku moja.

Wachezaji wa Yanga walipewa mapumziko ya siku moja ikiwa ni baada ya kushinda kwa bao 1-0 dhidi ya Toto African.
 
Yanga iko kileleni mwa ligi ikiwa imejihakikishia ubingwa huku Simba wakiamini watafanya miujiza.


Miujiza wanayosubiri Simba ni kushinda mechi ya mwisho kwa zaidi ya mabao matano dhidi ya Mwadui FC na Yanga wafungwe na Mbao FC ikiwezekana zaidi ya mabao matatu.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment