COPPA ITALIA: JUVENTUS YABEBA KOMBE MARA YA 12.

 COPPA-ITALIA-2017

JANA Mabingwa wa Italy Juventus wamebeba Coppa Italia kwa mara ya 12 ikiwa ni Rekodi kwa kuichapa Lazio 2-0 kwenye Fainali iliyochezwa Stadio Olimpico Jijini Rome huko Nchini Italy.
 
Kwa kubeba Kombe hili Juve sasa wamekamilisha awamu ya kwanza ya Trebo Msimu huu kwani Wikiendi hii inayokuja wanaweza kutetea vyema Ubingwa wao wa Serie A kwa mara ya 6 mfululizo na hapo Juni 3 wanaweza kutwaa Ubingwa wa UEFA CHAMPIONZ LIGI wakiwafunga Mabingwa Watetezi Real Madrid huko Cardiff, Wales.
 
Jana Bao za ushindi za Juve zilifungwa na Mabeki wao Dani Alves Dakika ya 12 na Leonardo Bonucci katika Dakika ya 24.
 
Juve, chini ya Kocha Massimiliano Allegri, wamekuwa Timu ya kwanza kubeba Coppa Italia mara 3 mfululizo.
Kwa Lazio hii ilikuwa ni Fainali yao ya 3 katika Miaka Mitano.
 
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment