MIFUPA YA GWIJI WA BRAZIL GARRINCHA HAIJULIKANI ILIPO.

Garrincha alifariki mwaka 1983
Garrincha alifariki mwaka 1983

Vyombo vya habari nchini Brazil vinasema kuwa mifupa ya gwiji wa zamani wa soka nchini humo Manuel Francisco dos Santos maarufu kama Garrincha, inaweza kuwa imepotea zaidi ya miongo mitatu baada ya kifo chake akiwa na miaka 49.

Kuna makaburi mawili ambayo yote yana majina yake mjini Rio de Janeiro lakini inawezekana kati ya hayo hakuna hata moja ambalo ni lake.

 Garrincha (kushoto) na Pele walitengeneza safu hatari ya ushambuliaji Brazil
Garrincha (kushoto) na Pele walitengeneza safu hatari ya ushambuliaji Brazil
Mmoja wa wahifadhi wa makaburi hayo anasema kuwa mifupa yake inaweza kuwa ilihamishwa miaka kadhaa iliyopita ila haijulikani wapi haswa ilipelekwa.

Garrincha mpinzani mkubwa wa Pele wa ni nani zaidi katika historia ya soka kwa nchi hiyo, aliisaidia nchi yake kutwaa kombe la dunia mwaka 1958 na 1962.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment