Kupitia Mtandao wa millardayo.com umeripoti
taarifa nzuri kwa soka la Bongo, ni kuhusu mtanzania Yohana Mkomola
anayeichezea timu ya taifa ya Tanzania ya vijana chini ya umri wa miaka
17 Serengeti Boys ambapo amethibitisha kupata dili la kwenda kuichezea
club maarufu ya soka ya Etoile du Sahel ya Tunisia.
Mkomola ni moja ya hazina ya wachezaji wanaochipukia kwa kuwa na kiwango kizuri akiwa uwanjani, hivyo kwa wapenzi wa soka la Tanzania tuitunze hazina hii.
MKOMBOLA KUSHOTO AKIWA TUNISIA. |
Mkomola aliitwa kwenda kufanya majaribio na timu hiyo amefuzu? mchongo aliupataje? anajibu “Habari
hizo ni kweli nilienda Etoile du Sahel kufanya majaribio katika timu
yao kwa wiki mbili lakini nilifanya kwa wiki moja na nusu tu nikapata
majibu kuwa nimefuzu.”
“Walikuwa
wananifatilia maana nilivyomaliza mechi na Congo meneja wangu
akaniambia kuwa kuna barua imekuja natakiwa kwenda kufanya majaribio
Etoile du Sahel ambapo nitajiunga na kikosi chao cha pili chini ya umri
wa miaka 20″ – Yohana
KIUNGO MSHAMBULIAJI INAMTAKIA KILA LA KHERI YOHANA MKOMOLA.
0 Maoni:
Post a Comment