JOHN TERRY AVUNJIWA NYUMBA YAKE.

  John Terry na Mkewe
Wezi wanaaminika kuvunja na kuingia katika nyumba ya aliyekuwa nahodha wa timu ya uingerewza John Terry wakati akiwa katika likizo ya kifamilia.

Maafisa wa polisi wa Surrey walithibitisha kwamba nyumba iliopo Oxshott ilivunjwa wikendi iliopita.

John Terry ameripotiwa kuishi katika nyumba ya vyumba saba nchini humo.

Msemaji wa kituo hicho cha polisi wa Surrey amesema kuwa : Tunaweza kuthibitisha kuwa wizi ulifanyika katika nyumba moja iliopo Moles Hill ,Oxshott usiku wa terehe 25 na 26 mwezi Februari.

Wezi hao wanadaiwa kuvunja na kuingia katika nyumba hiyo na kuiba vitu vyenye thamani wakati ambapo mchezaji huyo wa Chelsea mwenye umri wa miaka 36 alikuwa ameenda likizo na watu wa familia akiwemo mkewe Toni kulingana na ripoti za gazeti la The Sun.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment