ARSENE WENGER AMHOFIA BIG SAM.

Tokeo la picha la wenger vs big sam image
Arsene Wenger amekiri kuwa Mpinzani wake wa Siku nyingi Sam Allardyce, maarufu kama Big Sam, ni hatari kubwa katika azma ya Arsenal kufufua matumaini yao kwenye mbio za Ubingwa wa EPL, Ligi Kuu England.
 
Sam Allardyce hivi sasa ndio Meneja Mpya wa Crystal Palace ambayo Jumapili Januari Mosi, 2017, Siku ya Kwanza ya Mwaka Mpya, itazuru Emirates kucheza na Arsenal Mechi ya EPL.
Huko nyuma, wakati Allardyce akiwa Meneja wa Bolton Wanderers na West Ham, Wenger ashawahi kukwaruzana nae.

Hivi sasa Arsenal wako Nafasi ya 4 kwenye EPL na Mechi hii na Palace ni muhimu mno kwa Wenger na Arsenal yake kushinda ili wasitupwe mbali kwenye mbio za Ubingwa.
Lakini, kama ambavyo Wenger anavyotambua, Siku zote Timu za Big Sam hutumia miguvu na Mipira ya moja kwa moja bila kulemba ili kuwayumbisha Arsenal wanaopenda kumiliki mno Mpira.

Kwa Allardyce hii itakuwa Mechi yake ya Pili kuiongoza Palace tangu ateuliwe kuwa Meneja Wiki moja iliyopita na ya kwanza ilikuwa Droo ya 1-1 na Watford Siku ya Boksing Dei.
Nao Arsenal walishinda Mechi yao ya Boksing Dei 1-0 dhidi ya West Bromwich Albion kwa Bao la mwishoni lakini kabla ya hapo walichapwa Mechi 2 mfululizo na Everton na Manchester City.

Wenger, akiongea kuelekea Mechi hii na Palace, ameonyesha waziwazi kuihofia Mechi hii kwa kusema:  
“Ni muhimu mno kwa kila Timu kupigana kuwa juu. Baada ya kupata Meneja Mpya ni wazi Palace watajiamini zaidi na kuwa na mori zaidi. Hilo litafanya Gemu iwe ngumu mno. Chini ya Allardyce, Palace ni hatari mno!”

Arsenal wako Pointi 9 nyuma ya Vinara Chelsea na ushindi dhidi ya Palace ni kitu cha kufa na kupona kwao.

HALI ZA WACHEZAJI
Arsenal huenda wakamkosa Theo Walcott ambae ana maumivu ya Misuli ya Miguu akiungana na Majeruhi Kieran Gibbs mwenye tatizo la Goti lakini Sentahafu Shkodran Mustafi ameshapona tatizo la Misuli ya Pajani.
 Tokeo la picha la danny welback image
Pia Wenger ameshatoboa kuwa Fowadi wao Danny Welbeck amepona tatizo la Goti lililomuweka nje kwa muda mrefu na amerejea Mazoezini lakini kilichobaki ni kuamua ni wakati gani muafaka kuanza kumtumia tena.
Kwa upande wa Palace, wao watamkosa Beki wao Damien Delaney ambae yuko Kifungoni.

VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:

ARSENAL: Cech, Bellerin, Mustafi, Koscielny, Monreal, Coquelin, Xhaka, Sanchez, Ozil, Iwobi, Giroud
Akiba: Ospina, Martínez, Jenkinson, Gabriel, Holding, Elneny, Ramsey, Reine-Adélaïde, Sanogo, Pérez

CRYSTAL PALACE: Hennessey, MacArthur, Dann, Kelly, Ward, Flamini, Puncheon, Zaha, Cabaye, Townsend, Benteke
Akiba: Speroni, Fryers, Phillips, Wynter, Sako, Lee, Husin, McArthur, Ledley, Mutch, Campbell, Tomkins, Rémy
 Tokeo la picha la Andre Marriner image   Andre Marriner ndio refa atakayechezesha mechi hii kati ya Arsenal vs Crystal Palace.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment