LIVERPOOL YATOA KICHAPO KWA MAN CITY KUELEKEA MWAKA MPYA.

 Tokeo la picha la LIVERPOOL IMAGE
LIVERPOOL Jana imemaliza Mwaka 2016 kwa ushindi mtamu kwao Anfield walipoitungua Manchester City 1-0 na kubaki Nafasi ya Pili kwenye EPL, Ligi Kuu England, wakiwa Pointi 6 nyuma ya Vinara Chelsea.
 
Kipigo hiki kimewaacha City Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 4 nyuma ya Liverpool lakini wapo hatarini Leo kushushwa na Arsenal na Tottenham wakishinda Mechi zao.

Bao pekee na la ushindi kwenye Mechi hiyo lilifungwa Dakika ya 8 tu kwa Krosi ya Adam Lallana iliyounganishwa kwa Kichwa safi cha Georginio Wijnaldum.
 Tokeo la picha la LIVERPOOL IMAGE

LEO Januari Mosi zipo Mechi 2 za EPL kwa Watford kucheza na Tottenham na kisha Arsenal na Crystal Palace.

VIKOSI:

Liverpool: Mignolet, Clyne, Lovren, Klavan, Milner, Can, Henderson [Origi, 64’], Wijnaldum, Mane [Lucas, 89’], Lallana, Firmino.
Akiba: Karius, Sturridge, Moreno, Lucas, Origi, Ejaria, Alexander-Arnold. 

Man City: Bravo, Zabaleta [Jesus Navas, 86’], Otamendi, Stones, Kolarov, Fernandinho, Toure [Iheanacho, 89’], Sterling, Silva, De Bruyne, Aguero.
Akiba: Sagna, Fernando, Caballero, Jesus Navas, Clichy, Iheanacho, Garcia.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment