KOCHA WA "THE BLUES" ASEMA CHINA WAWE NA HESHIMA YA MATUMIZI YA FEDHA.

  Tokeo la picha la antonio conte image
www.kiungomshambuliaji.blogspot.com inakuletea hii; Kocha wa Chelsea, Antonio Conte anayejiita "the man himself" ambaye ameweka rekodi ya kipekee kwa kuwa kocha wa kwanza kuwa ndani ya Epl kwa msimu wa kwanza kushinda mechi 12 lakini pia kuvunja rekòdi ya Chelsea ya kushinda mechi 11 ameongelea kuhusu pesa zinazotolewa na Wachina.

Conte ambaye hivi karibuni amemruhusu Oscar kwenda nchini China katika klabu ya Shanghai SIPG inayofundishwa na Villa Boaz amesema 
 
"Wachina wanatoa pesa nyingi sana ukiangalia usajili wao wa Tevez ni
 pesa nyingi lakini pia kumtaka Ronaldo kwa pauni milioni 300 ni pesa
 nyingi zaidi Kulipwa mchezaji"

Tokeo la picha la antonio conte image
Conte alisisitiza kuwa "China wanapaswa kuheshimu pesa, si kutoa pesa tu bali kutoa kwa mpangilio mzuri. Ni ngumu mchezaji kukataa pesa wanazotoa China kwa kuwa ni nyingi sana"

Hivyo Conte hakubaliani na Pesa za Wachina anaona kama zinaharibu na hazijengi. Ikumbukwe sasa Wachina wameanza kumsaka mwamuzi Mark Clattenburg refa bora Duniani.
Tokeo la picha la Mark Clattenburg image
Mark Clattenburg
 
Na ni malengo yao kuitangaza ligi yao lakini pia kukuza soka lao ili waweze kubeba kombe la Dunia miaka ijayo.
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment