AZAM FC YAENDELEZA MAJIGAMBO KWA MAJI MAJI FC

  Tokeo la picha la PICHA WACHEZAJI WA AZAM
Azam FC ipo nafasi ya tatu na ina tofauti ya pointi 12 na vinara Simba katika Ligi Kuu Bara, sasa imejigamba leo ni lazima iwafunge Majimaji ugenini ili kupunguza utofauti wa pointi hizo.

Azam ina pointi 26 katika mechi 16 ilizocheza ambapo kati ya hizo, imeshinda mechi saba, imefungwa mara nne na imetoka sare mara tano, imefunga mabao 21 na imefungwa mabao 14.

Mchezo wa Azam na Majimaji unachezwa kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma na Ofisa Habari wa Azam, Jaffar Idd amesema: “Lazima tushinde.”

Timu hizo zinakutana katika Uwanja wa Majimaji leo ambapo Azam ina historia ya kutofungwa katika uwanja huo na wapinzani wao hao.

Akizungumza, Idd alisema wamejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo huo na ametamba wataendeleza ushindi wao kwa wapinzani wao hao ili wachukue pointi tatu muhimu.

“Kocha ameyafanyia marekebisho makosa yaliyojitokeza katika mechi yetu na African Lyon na tuna imani tutafanya vizuri katika mchezo wetu wa kesho (leo) ili kuweza kuendeleza rekodi yetu kwani hatujafungwa na Majimaji katika uwanja wao.

“Kikosi kipo vizuri na wachezaji wamejiandaa vizuri kuelekea mchezo huo isipokuwa tutawakosa wachezaji watatu ambao ni Daniel Amoah, Mudathir Yahaya na Gadiel Michael ambao ni majeruhi,” alisema Idd.


Kwa upande wake Kocha wa Majimaji, Kali Ongalla, alisema: “Mechi hii ni ngumu, wenzetu wana wachezaji wengi wa kigeni, ila tutapambana ili tushinde.”
 Tokeo la picha la WACHEZAJI WA MAJIMAJI PICHA
Share on Google Plus

About KASSIM OMARY

HII NI BLOG AMBAYO ITAKUWA INAKUPA HABARI MOTOMOTO ZA KIMICHEZO NA HABARI KWA UJUMLA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 Maoni:

Post a Comment